Soma Biblia

Contact Us

Use the form on the right to contact us.

Or use the information below to contact our main office in Dar es Salaam or Arusha.

Main office:

P.o. box 12772 Dar Es Salaam, Tanzania

Phone: +255 686 313 721 or +255 744 339 167

E-mail: manager.somabiblia@gmail.com

Publishing department

Postal address: P.o. Box 2696 Arusha, Tanzania

Phone: + 255 787392951

E-mail: publishingmanager.somabiblia@gmail.com

         

123 Street Avenue, City Town, 99999

(123) 555-6789

email@address.com

 

You can set your address, phone number, email and site description in the settings tab.
Link to read me page with more information.

Twende toleo la 1/2025 - 'Linapatikana'

Habari kutoka Soma Biblia

Twende toleo la 1/2025 - 'Linapatikana'

Cathbert Msemo

Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima
— Yohana 8:12).

MPENDWA MSOMAJI

Hapo zamani kijijini kwetu kulikuwa na miti mingi mikubwa pamoja na migomba na vichaka vidogo vidogo. Hapakuwa na maeneo ya wazi. Tena nyumba zilikuwa chache na hapakuwa na umeme.

Wakati wa usiku giza lilikuwa nene kila mahali kiasi cha kushindwa kutembea popote bila usaidizi wa mwanga. Hivyo tuliwasha taa au tochi na kutembea ikituongoza njiani tusijikwae na kuanguka. Tuliishi sehemu za milimani. Hivyo ukitazama nje usiku uliona karibu kila mahali penye njia taa zikimulika na watu kutembea.

Taa hizi zilimulika eneo dogo tu la njia, na ulihitaji kuwa makini usiteleze na kuanguka katika mlima.

Ninakumbuka hali hii jinsi ilivyokuwa ngumu. Lakini imenisaidia kuelewa ninapotafakari tofauti kati ya nuru iliyoletwa na taa zetu, na Nuru ya ulimwengu. Biblia inatufundisha juu ya Nuru hii. Ni nuru kuu na ya ajabu, maana si mwanga tu unaotupa kuona bali nuru hii inatupa uzima.

Nikukaribishe kusoma toleo hili kuhusu Nuru ya Ulimwengu. Makala zote zinafafanua vizuri jambo hili. Usisahau michezo pamoja na katuni. Pia katika Sala ya Vijana utajifunza jinsi unavyoweza kuwa kielelezo kwa wengine ili nao wavutwe kumfuata Yesu kama Bwana na Mwokozi wa maisha yao. Karibu tusome!

Nunua dukani Soma Biblia Dar es Salaam, Mbezi Luis, Arusha, Mbeya, Iringa, Mwanza,Dodoma