Karibu kununua TWENDE kwa Tsh. 500 tu katika maduka ya Soma Biblia. Toleo hili linafafanua juu ya Uhusiano wetu na Mungu. Kwa njia ya simulizi na hadithi nzuri utaweza kuelewa juu ya jambo hili. Utakutana pia na Dada Rehema na wenzake, na kuna michezo ya kuvutia. Usisahau kututumia majibu yako kama ilivyoelekezwa kwenye uk.5 na nyuma ya gazeti.
Read More
Mwaka mpya 2021 unakaribia. Umeshanunua kalenda ya ukutani? Soma Biblia tumekuandalia kalenda nzuri. Karibu kununua katika maduka yetu ya Soma Biblia
Read More
Karibu kusoma mpango wa Soma Biblia Kila Siku kwenye YouVersion bure.
Read More
Biblia ni taa ya miguu yake aishiye na Mungu. Soma Biblia tuna zana nzuri za kusoma Neno la Mungu kila siku. Soma Biblia kila siku 2021 ni Kalenda kamili na ufafanuzi kila siku kwa somo la Biblia
Karibu kununua nakala yako mapema katika maduka yetu ya Soma Biblia ili usichelewe kuanza mpango wa kusoma Biblia mwaka 2021.
Read More
Sisi wa Soma Biblia tunapenda kufanya kazi ya kuhubiri Injili kwa watoto bega kwa bega na Kanisa. Tuko tayari kuchangia ili furaha na baraka ya sikukuu ya watoto iendelee muda mrefu. Inawezekana ikiwa watoto wanapewa zawadi ya kudumu zaidi ya chakula kizuri.
Kwa hiyo tunatoa ofa maalumu ya vitabu fulani vinavyowafaa watoto pamoja na walezi wao wote wanaowafundisha imani na maisha ya Kikristo.
Read More
Katika toleo hili la RIZIKI tunaanza na mfululizo wa makala kuhusu Sala Kuu au Sala ya Bwana. Sala hii inatufundisha kuwa sifa zote, heshima na utukufu ni kwa Mungu wetu peke yake. Kazi yetu katika maisha ya hapa duniani na hata kifoni ni kumletea Mungu utukufu kwa kila tufanyalo. Sala hii ambayo unaweza kuiomba chini ya dakika moja inatuonyesha ukuu, urefu, upana na kina cha upendo wa Mungu kwetu kupitia Yesu Kristo.
Read More
Katika toleo hili tumefafanua zaidi jinsi Mungu anavyotutunza.
Read More
Ninakukaribisha usome makala zote na ujifunze mambo mazuri ya kujenga imani yako. Nikuambie! Mwaka huu Rehema atatoa zawadi kwa watoto watakaojibu vizuri maswali katika uk.5 na 6. Tazama katika ukurasa wa nyuma wa gazeti jinsi unavyoweza kutuma majibu yako. Majibu yako yakiwa sahihi, una kura moja. Tarehe 31/3, 30/6, 30/9 na 31/12 Rehema atatoa kura 15, yaani, kila mara kuna washindi 15 watakaozawadiwa.
Read More
Katika toleo hili la RIZIKI tunajadili namna tunavyoweza kufikia maisha kwa kuandaa viongozi walio bora kuanzia katika umri wa ujana. Nia ni kuliamsha kanisa kama taasisi muhimu na ya kuaminika katika kuandaa viongozi wenye hofu ya Mungu, wenye maadili mema, wachapa kazi na walio tayari kuacha maslahi yao kwa ajili ya wengine.
Read More
Katika toleo hili tutajifunza juu ya sauti ya Mungu. Je, unajua Mungu anatuita, na jinsi tunavyoweza kuisikia sauti yake na kuifuata? Karibu kusoma toleo hili uelewe vizuri zaidi.
Read More
Mambo vipi! Vijana, angalieni hapa, tumepata kifaa. Soma Biblia pamoja na Biblica Kenya tumezindua programu mpya ya vijana ijulikanayo kama FIKIA MAISHA. Sasa mambo ni poa kabisa.
Read More
Katika toleo hili la RIZIKI tunaangalia mada isemayo, “Ujenzi wa familia imara”. Lengo ni kuibua na kujadili changamoto zilizopo kwenye taasisi hii muhimu ambayo mwanzilishi wake ni Mungu mwenyewe pale bustani ya Edeni. Ni wito wa kuliamsha kanisa na jamii yote, kuwa taasisi hii inapaswa kulindwa, kuimarishwa na kupiganiwa kwa nguvu zote.
Read More
Mradi mpya wa kupeleka habari njema ya Yesu Kristo kwa vijana wanaokaa Arusha umeanza. Soma Biblia tumetembelea Shule ya Sekondari Sombetini na kuwagawia wanafunzi karibu na 1500 nakala ya kijitabu cha Masiha. Wote walipenda kupata zawadi hii.
Read More
Soma Biblia tuna mradi mpya wa kufikisha Injili kwa vijana kupitia kijitabu kinachoitwa Masiha. Kwa njia ya vibonzo, kijitabu hicho kinasimulia habari za Agano Jipya kuhusu maisha ya Yesu hapa duniani tangu kuzaliwa kwake mpaka alipopaa Mbinguni. Ni pamoja na mafundisho yake, na kusulubiwa, kufa na kufufuka kwake.
Read More
Sisi wa Soma Biblia tuna furaha ya kumkaribisha mkurugenzi mpya wa shirika letu, Mchungaji Bent Houmaa Jørgensen kutoka Denmark.
Read More
Usijinyime furaha ya kuwa na kitabu hiki kama msaidizi wako katika kazi uliyo nayo ya kufundisha mambo ya ndoa. Mwandishi mmoja wa Ndoa Yenye Furaha ni Askofu Blaston Gaville, KKKT Dayosisi ya Iringa, ambaye ana uzoefu mwingi wa kuwafundisha na kuwashauri wanandoa.
Read More
Katika toleo hili la RIZIKI tunajadili kurudi kwa Yesu kama alivyoahidi. Lengo ni kusaidiana kama kanisa kupeana maarifa yenye uhakika juu ya kuja kwa Yesu mara ya pili. Malengo ni wazi: Kwanza, tuwe na mafundisho sahihi kuhusu kurudi kwa Yesu. Pili, tuepukane na mafundisho ya uongo kuhusu jambo hili. Na tatu, tusije tukakata tamaa kuwa Kristo harudi, kisha tukalegea katika kuitenda kazi ya Mungu.
Read More
Mtoto mwenzangu, toleo hili lina habari njema kuhusu maisha yetu ya sasa na ya baadaye. Tutambue kwamba tukiwa ndani ya Yesu tutakuwa salama sasa na siku zijazo, na hata tukifa tutaenda kuishi na Yesu kwa furaha mbinguni.
Read More
Neno la Leo ni kitabu cha kubeba popote. Mistari 4 ya Biblia inatoa mwanga kila siku.
Read More
Soma Biblia kila siku 2020 ni Kalenda kamili na ufafanuzi kila siku kwa somo la Biblia
Read More